Kifo Cheusi Uingereza

Ramani ya Uingereza.
Kifo Cheusi Uingereza

Kifo Cheusi ilikuwa jina la pandemia ya ugonjwa wa tauni (kwa Kiingereza: bubonic plague) ambao uliwahi kuingia nchini Uingereza mnamo mwezi Juni 1348. Ilikuwa miongoni mwa dalili za awali za pandemia ya pili, iliyosababishwa na bakteria wa Yersinia pestis. Istilahi Kifo Cheusi haikutumika mpaka mwishoni mwa karne ya 17.

Asili au chanzo cha ugonjwa huu ni Bara la Asia, ila ulienea upande wa magharibi kipindi cha misafara ya biashara zilizozunguka Ulaya na uliwasili katika taifa la Uingereza Kusini-Magharibi kutoka kwenye jimbo la Gascony.

Ugonjwa huo wa tauni ulienezwa kwa kuambukizwa kupitia panya (flea-infected rats), vivyo hivyo pamoja na watu walioathiriwa na ugonjwa huo, panya walikuwa ni vekta wa Bakteria aina ya Yersinia pestis na Oriental rat flea walikuwa ni vekta wa awali.

Kisa cha kwanza kugundulika Uingereza kilikuwa cha baharia aliyewasili katika mji wa Weymouth, Dorset, kutoka Gascony mnamo mwezi juni 1348. Wakati wa kiangazi, ugonjwa wa tauni ulifika London, na wakati wa kipupwe pia ulisambaa katika lango la kuingilia Uingereza mnamo mwaka 1349, kabla hauja punguza kasi ilipofika mwezi Disemba, makadilio ya kiwango cha chini cha idadi ya vifo mwanzoni mwa karne ya 20 viliongezeka zaidi kutokana na kurudiwa kwa ukusanyaji mpya wa taarifa, kwa kiasi cha asilimia 40–60 ya idadi kubwa ya watu ilikubalika.

Matokeo ya awali yalikuwa yakipelekea kampeni ya mapambano kwa miaka mia moja. Kwa kipindi kirefu idadi ya watu ilipungua na kusababisha uhaba wa wafanyakazi, pamoja na kufuatiwa kwa kuibuka kwa malipo ya posho, ilipingwa na wamiliki wa ardhi, ambayo ilisababisha chuki ya hali ya juu miongoni mwa tabaka la chini. Mapinduzi ya wakulima wadogo wadogo ya mwaka 1381 kwa ujumla yalipelekea chuki kubwa , na hata hivyo uasi ulitokomezwa kwa kipindi kirefu cha utawala wa Kikabaila na ulikwisha kabisa nchini Uingereza. Kifo Cheusi pia kiliathiri juhudi za sanaa na utamaduni, na ilisaidia kuongeza matumizi ya lugha za asili.

Miaka 1361–1362 Ugonjwa wa tauni ulirejea nchini Uingereza, kwa kipindi hicho ulisababisha vifo kufikia asilimia 20 ya idadi ya watu. Baada ya hapo Ugomjwa wa tauni uliendelea kurejea kwa vipindi mpaka karne ya 14 na 15, kwa matokeo ya vijiji mpaka taifa zima kwa ujumla. Kufuatiwa na athari zake kwa uchache pamoja na mojawapo ya matokeo ya mwisho ya ugonjwa wa tauni nchini Uingereza ilikuwa ni ugonjwa wa tauni wa miaka 1665–1666 jijini London.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search